mtoto.news

Akamatwa kwa Tuhuma za Usafirishaji Haramu wa Watoto

September 7, 2022

Polisi nchini Nigeria wamemkamata mwanamke mwenye umri wa miaka 44 kwa tuhuma za wizi wa watoto 15 katika jimbo la kusini la Rivers.

Polisi wanasema kwamba, watoto hao walitekwa nyara ili kuuzwa na mwanamke huyo , ambaye alidai kuwa yeye ni mtawa anayeendesha kituo cha watoto yatima.

Watoto hao wanaripotiwa kuwa na umri wa kati ya miaka minne na 15.

Polisi walisema kuwa, wanajitahidi kuwaunganisha watoto hao na wazazi wao.

Hey, like this? Why not share it with a buddy?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *