mtoto.news

Mipango ya Kuondoa makazi ya watoto na yatima imeng'oa Nanga

November 11, 2022

 

Mkakati wa Marekebisho ya Utunzaji uliopangwa wa miaka 10 unalenga kutoa masuluhisho mbadala kwa malezi ya watoto na kutilia mkazo ukweli kwamba familia itasalia kuwa kitengo muhimu katika malezi ya mtoto.

Afisa wa kurugenzi ya kitaifa ya Huduma za Watoto Jane Munuhe akiwahutubia wasimamizi wa nyumba za watoto na vituo vya watoto yatima katika mji wa Kakamega. Aliwaeleza kuhusu vifungu vya Sheria Mpya ya Watoto, 2022 na utoaji wa Mkakati wa Marekebisho ya Matunzo ya Kitaifa huku serikali ikiweka mipango ya kufunga nyumba zote za watoto na yatima katika miaka 10. Picha: Purity Simiyu/ KNA.

 

Mkurugenzi msaidizi anayeshughulikia Malezi na Mageuzi katika Kurugenzi ya Huduma za Watoto Jane Munuhe amesema kwamba, serikali imetunga sheria mpya. Akizungumza mjini Kakamega siku ya Alhamisi , alisema kwamba, Sheria ya Mtoto ya 2022 inatoa muda wa miaka 10 kwa Kenya kukomesha makazi ya watoto na yatima.

“Kenya imetia saini Mkataba na Itifaki za Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watoto na pamoja na sheria za mitaa, familia na jamii zinasalia kuwa njia bora zaidi ya malezi ya watoto,” Munuhe alisema. “Sheria hii mpya ya watoto inaunga mkono haki za watoto kukua katika familia na jamii.”  Munuhe, ambaye alizungumza na mameneja na wafanyakazi wa kijamii wa vituo vya kulelea watoto yatima na kulelea watoto alisema kwamba, hiyo ni sehemu ya mafunzo ambayo Idara ya Huduma za Watoto inashiriki, ili kuwaandaa kwa ajili ya mpito ambao umepitishwa duniani kote.

“Wanafunzwa wanachukuliwa kupitia vifungu vya Sheria ya Mtoto na mkakati wa marekebisho ya malezi. Lengo ni kwamba wakishapata maarifa wataweza kuanzisha mchakato wa kuhakikisha kwamba watoto wanarejea kwa familia zao na jamii,” alisema.

Aidha, Afisa huyo alisema kuna watoto 45,000 -50,000 wanaoishi katika  taasisi takriban 855 za watoto za hisani na wengine wanaishi katika taasisi zinazosimamiwa na serikali.  Aliwashauri wakufunzi wa Kakamega kufanya uchanganuzi wa hali ya watoto kwa sababu itaonyesha ukubwa wa tatizo ambalo watakuwa wakikabiliana nalo wanapoanza mchakato wa mageuzi ya malezi.

Munuhe alifafanua kwamba, kwa wale watoto ambao hawana makazi, au ni yatima au waliotenganishwa na wazazi wao watapatiwa programu ya malezi mbadala ya familia ambayo ni pamoja na malezi ya jamaa, malezi ya kambo, ulezi, kuasili na mengine mengi.

Hey, like this? Why not share it with a buddy?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *