mtoto.news

Goma DRC: Nasaha ya Uhuru Kenyatta Juu ya Kuwaepusha Watoto na Vita.

November 16, 2022

Rais wa zamani wa Kenya Uhuru Kenyatta (katikati) akiwasili Goma, mashariki mwa DRC mnamo Novemba 15, 2021. Aliwasihi wapiganaji wakomeshe vita huko Kivu Kaskazini alipokutana na watu waliokimbia makazi yao wakitoroka mapigano. PICHA | ALEXIS HUGUET | AFP

Rais wa zamani wa Kenya Uhuru Kenyatta Jumanne alienda karibu na eneo la vita huko Goma na Rutshuru, Kivu Kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambapo aliwasihi wapiganaji kukomesha vita huku akikutana na watu waliokimbia makazi yao wakitoroka mapigano.

Bw Kenyatta, ambaye ni mpatanishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yenye nchi saba, alialikwa katika Kituo cha Uratibu wa Uendeshaji wa Pamoja kabla ya kuchukua barabara ya Rutshuru, ambayo iko maeneo ya IDP.

Mkuu huyo wa zamani wa nchi ya Kenya alishtushwa na hali aliyoiona na kulaani vikali janga la kibinadamu linalowakabili watu wa Kivu Kaskazini.

“Tumeona watoto pamoja na akina mama na wazee wanakuwa wageni katika nchi yao. Tunafaa kutupilia mbali tofauti zetu, na kuwaonea huruma na tuache vita,” alisema kwa hisia kali.

Bw Kenyatta alizungumza na wapiganaji waliokimbia makazi yao ambao walilalamikia hali ya hatari wanayoishi.

Familia nyingi zinawasili makazi hayo ya wakimbizi kila siku kutoka Rutshuru, hasa kutoka kwa vikundi vya Kibumba na Muhumba, na wanakaa katika shule, makanisa na maeneo ya umma katika eneo la Nyragongo huko Kivu Kaskazini.

Kulingana na Constant Ndima, gavana wa kijeshi wa Goma, kuna takriban watu 38,440 waliokimbia makazi yao wakiwemo watoto. Tangu kuanza kwa mapigano hayo, zaidi ya watu 200,000 tayari wamekimbia maeneo yao.

Siku ya Jumanne, mamia ya watu walimiminika mjini Goma, kufuatia hofu iliyozushwa na kengele ya uongo iliyotangaza kuwepo kwa waasi katika mji huo.

Hey, like this? Why not share it with a buddy?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *