mtoto.news

Vikwazo, Shule Zinapofunguliwa

January 23, 2023

Picha : Thomas Mukoya/Reuters

Shule zote zilizo Afrika Mashariki zinaanza muhula wa kwanza mwaka huu, huku zikikumbatiwa na hali ya kusumbua ya mara kwa mara ya kutafuta rasilimali ili kuhakikisha kwamba, elimu haina gharama kubwa. Kutoka Tanzania hadi Rwanda, Kenya na Uganda, msururu wa vifaa duni vya kujifunzia, walimu, msongamano wa wanafunzi na mkanganyiko wa ada utatawala wiki hii ya ufunguzi wa muhula mpya.

Kwa kuzingatia utekelezwaji wa mageuzi ya Rais William Ruto nchini Kenya, kuhusu elimu ambapo wataalam walikadiria yatagharimu angalau Kshs bilioni 635  kwa miaka mitano, Rais ako tayari kujifunga kitita wakati wa mwaka wake wa kwanza ambapo elimu ipo chini ya uongozi wake.

Mnamo wiki hii, shule nchini Kenya zinafunguliwa, huku kukiwa na mkanganyiko kuhusu upangaji wa wanafunzi wa shule ya upili (JSS) katika Mtaala mpya wa Ustadi (CBC), ambao umekumbwa na mkanganyiko na mipango duni. Huku Tume ya Utumishi wa Walimu ikiharakisha kuajiri walimu ili kuziba mapengo ya wafanyakazi, Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu alisema wiki iliyopita kwamba serikali itatoa fedha ili kuwezesha mpango wa shule za upili kuenda sambamba.

Ujenzi wa miundombinu

Kenya inatenga Ksh15,000  kwa kila mwanafunzi wa JSS, na kutoa msukumo mkubwa kwa shule za msingi ambazo zitawawezesha kuimarisha ujenzi wa maabara, madarasa na kupata vifaa vya elimu.

“Tumeshughulikia takwimu iliyo karibu na ile inayotolewa kwa shule za upili ambayo ni takriban Ksh22,240,” Machogu alisema Jumatatu wiki ilyopita alipokuwa akizindua uteuzi wa kidato cha kwanza jijini Nairobi.

Jukumu la haraka ni kuajiri walimu, kwa shule za sekondari na msingi, ambapo serikali imejitolea kuziba upungufu wa 116,000. Hii itagharimu angalau Ksh bilioni 238 . Serikali pia inakabiliwa na shinikizo la kifedha la kukusanya Ksh bilioni 28.84 ili kuboresha uwezo wa shule za kutwa, kuhakikisha upatikanaji wa elimu bora na kupunguza gharama zao huku msongamano ukizidi kuwa mbaya katika taasisi za masomo.

Hivi majuzi rais alisema kuwa wanafunzi wa shule za upili ambao hawana maabara katika shule zao watapewa fursa ya kupata hizi katika shule jirani. Lakini kinacholeta changamoto kubwa ni ufichuzi wa Ofisi ya Bunge ya Bajeti katika ukaguzi wake wa sekta ya elimu kwamba asilimia 50 ya shule za sekondari za bweni na asilimia 70 ya shule za kutwa hazina vifaa vya maabara.

Hii inaiacha serikali bila chaguo ila kujenga vifaa, mradi wa muda mrefu ambao unaweza kuchukua miaka ili kukamilika.

Mahitaji makubwa ya kifedha

Ingawa utawala uliopita ulikuwa na wasiwasi kuhusu gharama ya kutekeleza mtaala wa CBC, mapendekezo katika manifesto ya Kenya Kwanza kuhusu kuleta mageuzi katika sekta ya elimu yanatoa taswira ya mahitaji makubwa ya kifedha ambayo serikali inakabiliana nayo.

Jaribio la tindikali kwa utawala wa Ruto, hata hivyo, ni kuhakikisha mabadiliko ya asilimia 100 ya wanafunzi 1,287,597 waanzilishi wa Darasa la Sita, waliofanya Tathmini ya Elimu ya Shule ya Msingi ya Kenya mwaka jana, hadi shule ya upili ya chini ambayo ina Darasa la Saba, Nane na Tisa.

Nchini Tanzania shule zimefunguliwa tena huku kukiwa na uhaba wa walimu, madarasa na nyenzo za kujifunzia, hasa vifaa vya maabara na vitabu. Jumla ya watoto 1,073, 941 waliokaribia kugawiwa sawasawa kati ya wavulana na wasichana, wamechaguliwa kuanza masomo ya kidato cha kwanza wiki hii chini ya agizo la serikali ya Tanzania la kutoa elimu bure kwa watoto wote wanaomaliza shule ya msingi.

Hey, like this? Why not share it with a buddy?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *