mtoto.news

Wizara yawashinikiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto shuleni

March 6, 2023

 

Serikali inatafuta mamia ya watoto ambao bado hawajajiunga na shule za upili licha ya kupokea barua za kujiunga na shule hizo.

Katika azma yake ya kufikia mabadiliko ya asilimia 100 kutoka shule ya msingi hadi ya upili, Utawala wa Serikali ya Kitaifa na Wizara ya Elimu wanapanga kufanya msako wa nyumba hadi nyumba, ili kuwatafuta wanafunzi waliopotea ambao walifanya mtihani wao wa Cheti cha Elimu ya Sekondari nchini Kenya mwaka jana.

Kundi la viongozi katika kaunti ya Narok na Kilifi wanaunga mkono mpango huo na kuwataka polisi kuwakamata wazazi wanaowaweka watoto wao nyumbani. Kamishna wa kaunti ya Narok Isaac Masinde alisema kwamba, wanafunzi 1,200 hawajulikani waliko, akiongeza kuwa idadi ya shule za upili za kaunti ni asilimia 93. “Asilimia nyingine saba hawajaripoti licha ya serikali kutangaza elimu ya sekondari ya kutwa bila malipo,” Masinde alisema.

Hata hivyo, hakutoa mchanganuo wa idadi ya wasichana na wavulana kwenye orodha ya wanafunzi ambao hawajaenda shuleni. Masinde alilaumu mabadiliko ya chini ya shule za msingi hadi sekondari kutokana na ukosefu wa taarifa kwamba serikali inatoa elimu ya sekondari bila malipo katika shule za kutwa.

Ili kufanikisha mabadiliko hayo ya asilimia 100, kamishna huyo wa kaunti alisema kuwa, wasomi, viongozi wa kisiasa na makasisi lazima washirikiane. “Tunataka kuwafahamisha wazazi kuwa elimu ya sekondari ni bure na vitabu vya kiada pia ni bure. Wanachohitaji ni kununua sare za mtoto za shule na kutoa pesa za chakula cha mchana,” alisema.

Juu ya Sekondari ya Vijana, Masinde alinena serikali itashirikiana na wazazi, walezi na viongozi kufikia mabadiliko ya asilimia 100“Ni jukumu letu kama wazazi na viongozi kuhakikisha kila mtahiniwa aliyefanya tathmini katika darasa la sita anapitia darasa la saba,” Masinde alisema.

Mjini Kilifi, kiwango cha mpito cha kitaifa kilifikia asilimia 95. Kwale na Kilifi walikuwa na asilimia 30 ya watoto ambao walikuwa bado nyumbani kufikia wiki iliyopita. Wakiongozwa na MCA wa Ganda Oscar Wanje, kundi la viongozi mjini Kilifi walisema kwamba wazazi wengi wamewatelekeza watoto wao na wanaingilia kiwango cha mpito kinachoenezwa na serikali.

Wanje aliwatahadharisha wazazi katika wadi yake kuwa hatawaokoa iwapo watakamatwa kwa kukosa kuwapeleka watoto wao shuleni. “Kuna waraka kutoka kwa serikali kwamba watoto wote wanafaa kwenda shule hata kama watakuwa hawana karo ya shule au sare. Acha watoto wote walio na matatizo ya karo ya shule waletwe ofisini kwangu kwa usaidizi,” alisema.

MCA aliyeteuliwa Betty Kache alisema kuwa, serikali inafaa kuwakamata wazazi kama mfano kwa wale wanaokataa kuwapeleka watoto wao shuleni. “Itakuwa funzo kwa wengine iwapo polisi watawakamata wazazi wawili au watatu kwa kutopeleka watoto wao shule,” alisema.

Aidha Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu alisema kwamba, kaunti kama vile Kilifi na Kwale ziko nyuma katika mabadiliko ya watoto kutoka shule ya msingi hadi ya upili na kwamba maafisa wa wizara hiyo wataungana na wenzao kutoka wizara ya Mambo ya Ndani ili kuchunguza kinachogaubaga.

Hey, like this? Why not share it with a buddy?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *