mtoto.news

Kifungo cha Maisha kwa Kosa la Kunajisi Mtoto Nchini Kenya

March 16, 2023

Ripoti ya hivi majuzi ya

Ofisi ya Kitaifa ya Takwimu ya Kenya inaonyesha kuwa msichana mmoja kati ya wanne na mvulana mmoja kati ya kila mvulana tisa hudhulumiwa kingono kabla ya kufikisha umri wa miaka 18.

Ripoti hiyo pia inafichua kuwa ni asilimia 41 tu ya wanawake na asilimia 39.2 ya wanaume waliokumbana na aina yoyote ya ukatili ndio walioweza kufichua masaibu yao. Kinachoshangaza zaidi kuhusu matokeo ya KNBS ni ukweli kwamba hatari ya Unyanyasaji wa Kijinsia (SGBV) ni kubwa zaidi kwa watoto wanaoishi katika umaskini na kwa wale ambao wamepitia aina nyingine za unyanyasaji katika nyumba zao au jamii.

Watoto wengi wanaopitia aina yoyote ya unyanyasaji  wanaogopa kuongea haswa ikiwa wanashuku kuwa hawako katika mazingira salama kwao kufunguka. Cha kusikitisha ni kwamba, watoto wengi hudhulumiwa na kunyanyaswa kijinsi na watu wao wa karibu.

Aidha, mara nyingi wengi wetu huzingatia mtoto wa kike na kusahau kuhusu wavulana, kwani ukweli wa kusikitisha ni kwamba kuna wavulana wanaodhulumiwa kingono na kudhulumiwa kimwili lakini tofauti pekee ni kwamba wavulana hawaongei wanapodhulumiwa.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 8(2) cha Sheria ya Makosa ya Kujamiiana ya mwaka 2006 mtu yeyote atakayetenda kosa la kunajisi mtoto mwenye umri wa miaka kumi na moja au chini ya hapo akitiwa hatiani atahukumiwa kifungo cha maisha.

Kifungu cha 8(3) cha sheria hiyo hiyo pia kinaeleza kuwa mtu yeyote anayetenda kosa la kunajisi mtoto mwenye umri wa kati ya miaka 12 hadi 15 atawajibika kwa adhabu ya kifungo kisichopungua miaka 15 jela.

Hata hivyo licha ya adhabu kali zilizoelezwa katika sheria, kesi za unajisi nchini Kenya zimekuwa zikiongezeka kwa miaka mingi, na kuleta changamoto kubwa kwa mfumo wa kijamii na kimaadili nchini.

Hey, like this? Why not share it with a buddy?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *