mtoto.news

Categories
Health Latest News

Dawa za sharubati zapigwa marufuku baada ya vifo vya watoto 99.

Vifo vya karibu watoto 100 nchini Indonesia vimesababisha nchi hiyo kusimamisha uuzaji wa dawa zote za sharubati. Ni wiki chache tu baada ya dawa ya kikohozi nchini Gambia kuhusishwa na vifo vya karibia watoto 70. Indonesia imesema kwamba, baadhi ya dawa za sharubati zimepatikana kuwa na viambato vinavyohusishwa na majeraha ya figo (AKI), ambayo yameua […]

Categories
Uncategorized

Wakenya 31 waokolewa kutoka kwa wateka nyara huko Laos

Mnamo tarehe 31 Agosti 2022, HAART{Ufahamu Dhidi ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu}ilipokea ombi la kutaka usaidizi kupitia mitandao ya kijamii na barua pepe. Bwana mmoja aliwafahamisha HAART kwamba mwanafamilia wake ameshawishiwa kwa ahadi za uwongo za kufanya kazi Thailand ila alisafirishwa hadi Laos, pamoja na Wakenya wengine. Kwa hofu, Bwana huyo aliiomba HAART kuingilia kati […]

Categories
Education

Lamu: Hofu baada ya mimba za mapema kushika kasi

Mimba za mapema sio jambo geni nchini Kenya, ila kwa sasa, wakaazi wa maeneo ya Hindi huko Lamu wameonya hofu na wasiwasi mkuu baada ya wanafunzi sita kutoka shule ya upili ya Hindi kupachikwa mimba kwa pamoja. Kulingana na citizen, Wasichana wadogo wanapitia dhulma mbali mbali maeneo ya Hindi ikiwemo kupachikwa ujauzito wa mapema, – […]

Categories
Education Education education Latest News

Makali ya Njaa yawaweka watoto nje ya madarasa

Shuleni Kavunzoni, watoto wengi wanalilia njaa huku wengi wao wakikosa kuwa makini darasani, ni misimu minne sasa isiyo na mvua mjini Ganze kaunti ya kilifi. Udongo umemumunyuka na ardhi imekomaa, watoto hawapati chajio wala kiamsha kinywa. Imekadiria miaka mitano sasa, ambapo wenyeji hawajaweza kupanda wala kuvuna chochote kile,ila hio ndio hali ambayo watoto kama Moses […]

Categories
Education Education education

Gachagua: CBC haiendi popote

Naibu Rais Rigathi Gachagua amethibitisha kuwa Mtaala wa Kuzingatia Umahiri (CBC) hautafutiliwa mbali. Akizungumza Jumatano katika Taasisi ya Utafiti ya Cemastea, Gachagua alisema kwamba, serikali itaboresha zaidi CBC. “CBC haiendi popote, haijafutwa bali itaboreshwa tu,” alisema. Aliongoza uzinduzi wa siku tatu za kuanzishwa kwa Kikosi Kazi cha Marekebisho ya Elimu. Jopokazi la wanachama 49 liliundwa na Rais William […]

Categories
Uncategorized

Tuwalinde watoto dhidi ya ukatili

Ndani ya mwaka mmoja, takriban watoto bilioni moja wananyanyaswa kote ulimwenguni. Kila mwanadamu, bila kujali kabila, cheo, dini, elimu, au hali yoyote ile, ana haki ya kuishi katika ulimwengu wenye amani na usio na kila aina ya vurugu. Hata hivyo, kuna haja ya dharura ya kuchukuliwa kwa hatua zaidi za kuzuia na kukabiliana na tishio […]

Categories
Uncategorized

Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike:”Haki zetu, Mustakabali wetu”

Mnamo 2022, tunaadhimisha kumbukumbu ya miaka kumi tangu kuzaliwa kwa Siku ya Kimataifa ya Msichana (IDG). Katika miaka hii 10 iliyopita, kumekuwa na umakini mkubwa katika masuala ambayo ni muhimu kwa wasichana, haswa miongoni mwa serikali, watunga sera na umma kwa ujumla, pia kumekuwa na umuhimu chanya katika kuwapa wasichana fursa zaidi kwa kusikilizwa sauti zao katika […]

Categories
Education Education education Latest News

Kenya: Wadau wa Elimu Wajitolea Kufundisha usimbaji(coding)Shuleni

Chama cha Shule za Kimataifa cha Kenya (KAIS) kwa ushirikiano na kampuni ya Education Technologies, Kodris Africa na Kenya Commercial Bank waliitisha kongamano la ujuzi wa Kidijitali mnamo Alhamisi lililowaleta pamoja wadau mbalimbali kutoka sekta ya elimu na ICT. Tukio hilo lilijikita katika mtaala wa kompyuta na usimbaji (coding)na umuhimu wa kujumuisha ujuzi wa kidijitali […]

Categories
Health Latest News

Vifo vya watoto nchini Gambia vimehusishwa na dawa za kikohozi zilizotengenezwa India

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa tahadhari hapo Jumatano kuhusu dawa nne za kikohozi na baridi zilizotengenezwa na Maiden Pharmaceuticals nchini India, na kuonya kuwa zinaweza kuhusishwa na vifo vya watoto 66 nchini Gambia. Shirika la afya la Umoja wa Mataifa pia limetahadharisha kwamba dawa zilizoambukizwa huenda zilisambazwa nje ya nchi hiyo ya Afrika Magharibi, […]

Categories
Uncategorized

Sudan: Mafuriko, mashambulizi ya wanamgambo na njaa yatatiza masomo ya watoto

Kufuatia mvua kubwa na mafuriko nchini Sudan, makumi ya maelfu ya nyumba, visima na mashamba ya kilimo yameharibiwa huku familia 80,000 zikihitaji msaada wa kibinadamu makadirio ya Hilali Nyekundu ya Sudan (SRCS). Mashirika ya misaada yameonya kwamba, takriban kila mtoto aliye na umri wa kwenda shule nchini Sudan anakosa elimu, Baadhi ya majimbo nchini Sudan, […]